Mwanasayansi wa Syria auawa mjini Damascus, hofu yatanda baada ya kuondolewa madarakani Assad
Mwanasayansi wa Syria auawa mjini Damascus, hofu yatanda baada ya kuondolewa madarakani Assad Dec 12, 2024 04:11 UTC Watu wenye silaha wamemuua mwanasayansi mashuhuri wa Syria mjini Damascus huku kukiwa na hofu ya kufanyika msako dhidi ya wasomi wa nchi hiyo baada ya kuondolewa madarakani serikali ya Syria hivi karibuni na makundi yenye silaha yanayoungwa mkono na mataifa ya kigeni, hasa madola ya Magharibi. Dakta Hamdi Ismail Nadi, ambaye alikuwa amebobea katika kemia ya hali ya juu na dawa, alipatikana amekufa nyumbani kwake katika mji mkuu wa Syria siku ya Jumanne. Taarifa zinasema kifo cha Nadi ni cha kushangaza kwani hapo awali alijulikana kama msomi wa ngazi za juu katika uwanja wake na alikuwa na michango muhimu katika utafiti wa ndani na wa kimataifa katika uga wa kemikali. Habari ya kuuawa Dakta Nadi imeleta mshtuko katika jamii ya wanasayansi na wasomi nd...