Israel yasema 'hatua zimepigwa' kusitisha mapigano Lebanon

 

Israel yasema 'hatua zimepigwa' kusitisha mapigano Lebanon

Saa 18 zilizopita

Israel kupitia kwa waziri wake wa mambo ya nje, Gideon Saar, imeeleza kuwa kuna maendeleo fulani kuelekea usitishaji mapigano nchini Lebanon.

https://p.dw.com/p/4mtFy
Nakili kiunganishi
Israel inaendeleza mashambulizi Lebanon dhidi ya Hezbollah
Vita vimerindima kwa zaidi ya wiki sita nchini Lebanon wakati Israel ikiwalenga wapiganaji wa Hezbollah.Picha: Nidal Solh/AFP

Saar ametoa kauli hiyo mjini Jerusalem wakati alipoulizwa swali na waandishi wa habari, kuhusu uwezekano wa kusitishwa vita. Mwanadiplomasia huyo amejibu ya kwamba kuna hatua kadha zimepigwa na wanashirikiana na Marekani katika suala hilo.

Soma pia: Mashambulizi ya Israel yauwa zaidi ya watu 20 Lebanon

Hata hivyo, kundi la Hezbollah, limedai kwamba halijapokea mapendekezo yoyote kuhusu makubaliano ya usitishaji vita nchini Lebanon.

Msemaji wa kundi hilo, Mohammad Afif, ameeleza kwamba hadi kufikia sasa hakuna taarifa rasmi iliyowafikia lakini anaamini bado wamo katika hatua za kuwasalisha mapendekezo ya awali na majadiliano ya kina. Israel iliongeza mashambulizi ya anga mwishoni mwa mwezi Septemba yakilenga ngome za Hezbollah kote Lebanon.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan