Putin asema vita vya Ukraine vinachukua mkondo wa kidunia

 

Putin asema vita vya Ukraine vinachukua mkondo wa kidunia

Saa 3 zilizopita

Rais Vladimir Putin amesema vita vya Ukraine vinageuka kuwa mgogoro wa kidunia. Hii ni baada ya Marekani na Uingereza kuiruhusu Ukraine kuishambulia Urusi na silaha inazopewa na nchi hizo.

https://p.dw.com/p/4nIRg
Nakili kiunganishi
Rais wa Urusi Vladimir Putin
Putin amezionya nchi za Magharibi kuwa Moscow inaweza kujibu mashambuliziPicha: Vyacheslav Prokofyev/Sputnik/Kreml Pool/AP/picture alliance

Putin amezionya nchi za Magharibi kuwa Moscow inaweza kujibu mashambulizi hayo. Ametangaza kuwa Urusi imetumia aina mpya ya kombora la masafa ya kati, kushambulia kituo cha kijeshi cha Ukraine. Putin amesema, baada ya idhini kutoka kwa serikali ya Joe Biden, Ukraine iliipiga Urusi na makombora sita yaliyotengenezwa na Marekani aina ya ATACMS mnamo Novemba 19 na makombora ya Uingereza ya Storm Shadow Novemba 21.

Soma pia: Zelensky adai Putin aigeuza Ukraine uwanja wa majaribio ya silaha zake

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametoa wito kwa viongozi wa dunia kujibu vikali matumizi ya Urusi ya kombora jipya la masafa marefu. Amesema hatua hiyo ya Urusi inaongeza kiwango cha ukatili katika vita vyake dhidi ya Ukraine. Zelensky amesema huo ni ushahidi wa mwisho kuwa Urusi bila shaka haitaki amani.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan