Rais wa zamani Macky Sall analenga kurejea tena katika siasa za Senegal
Rais wa zamani Macky Sall analenga kurejea tena katika siasa za Senegal
Rais wa zamani wa Senegal Macky Sall, analenga kurejea tena katika ulingo wa kisiasa katika uchaguzi wa dharura wa wabunge ulioratibiwa kufanyika siku ya Jumapili.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Sall ambaye kwa sasa anaishi nchini Morocco, aliondoka madarakani mwezi Aprili mwaka huu baada ya kuongoza kwa kipindi cha miaka 12, akimuachia uongozi mrithi wake Bassirou Diomaye Faye.
Rais wa zamani kwa sasa anaongoza muungano mpya wa upinzani akiwa katika nchi ya kigeni, suala ambalo wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanahoaji nia yake ya kutaka kurejea tena kwenye siasa za taifa hilo la Afrika Magharibi.
Waziri Mkuu wa sasa wa Senegal, hasimu wa kisasa wa Sall, Ousmane Sonko, ameendelea kusisitiza kwamba wanasiasa wote waliokuwa katika utawala wa zamani huenda wakafunguliwa mashtaka.
Sonko amekuwa akiutuhumu utawala wa Sall kwa kuhusika na ubadhirifu wa pesa za umaa, madai ambayo hata hivyo viongozi wa zamani wametupilia mbali.
Mchambuzi na mtaalam wa masuala ya kisiasa professa Maurice Soudieck Dione anasema hatua ya Sall kurejea kwenye siasa ni njia moja ya kulinda masilahi yake iwapo kungetokea athari zozote za kisiasa dhidi yake.
Sall alihairisha uchaguzi mkuu wa urais wa mwezi Februari, hatua ambayo ilizua mzozo mkubwa wa kisiasa nchni Senegal. Licha ya Sall kumpendekeza Amadou Ba, kumrithi kwenye uchaguzi huo, mgombea wake alipoteza dhidi ya naibu wa zamani wa Sonko Faye.
Faye na Sonko waliachiwa kutoka gerezani siku kumi kabla ya uchaguzi mkuu wa urais. Rais Faye alivunja bunge ambalo lilikuwa na idadi kubwa ya wapinzani mwezi Septemba na kutoa nafasi ya kufanyika kwa uchaguzi mpya wa wabunge.
Comments
Post a Comment