Senegal: Chama cha rais Faye kimepata idadi kubwa ya viti vya ubunge
Senegal: Chama cha rais Faye kimepata idadi kubwa ya viti vya ubunge
Chama tawala nchini Senegal, Pastef, kimeshinda karibu robo tatu ya viti vya ubunge katika uchaguzi uliofanyika wikendi iliyopita, matokeo yanayomaanisha kuwa sasa sera za Serikali mpya zitapitishwa kirahisi.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa matokeo ya awali, chama cha rais Bassirou Faye kimepata wabunge 130 kati ya 165 wanaotakiwa katika bunge la kitaifa, matokeo yaliyothibitisha na maofisa wa chama tawala.
Matokeo haya hata hivyo yatasalia kuwa ya awali hadi pale yatakapothibitishwa na mahakama ya kikatiba ndani ya siku 5 zijazo.
Ikiwa ushindi huu wa chama cha Pastef utathibitishwa na mahakama, utakuwa ushindi mkubwa zaidi katika historia ya chaguzi za taifa hilo kwa chama kimoja kufikisha wabunge zaidi ya 120.
Upinzani uliokuwa unaongozwa na rais wa zamani Macky Sall, uliambulia wabunge 16, huku chama cha waziri mkuu wa zamani Amadou Ba kikipata viti 7 na viti vitatu vilienda kwa aliyekuwa meya wa Dakar Barthelemy Dias.
Comments
Post a Comment