Katika miezi tisa iliyopita Yemen imeshambulia meli 170 za Marekani na Wazayuni
Katika miezi tisa iliyopita Yemen imeshambulia meli 170 za Marekani na Wazayuni
Aug 08, 2024 06:32 UTC
Tovuti ya habari ya Yemen imetangaza katika ripoti yake kuwa katika kipindi cha miezi tisa iliyopita vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo vimezishambulia meli 170 za Wamarekani na Wazayuni.
Almasirah imeeleza katika ripoti yake iliyochunguza
operesheni zilizofanywa na vikosi vya ulinzi vya Yemen kati ya Novemba
2023 hadi Julai mwaka huu kwamba katika operesheni hizo, vikosi hivyo
vimezilenga meli zipatazo 170 zenye uhusiano na adui Mzayuni.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, meli 41 kati ya zilizopigwa zilikuwa za
adui wa Kizayuni, meli 72 za Marekani na meli 12 zilikuwa za Uingereza.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa, kati ya hizo zote, karibu meli 45
zimeshambuliwa na jeshi la Yemen kutokana na kukiuka marufuku ya kuingia
katika bandari za utawala wa Kizayuni katika ardhi zinazokaliwa kwa
mabavu za Palestina.
Almasirah imemalizia ripoti hiyo kwa kubainisha kuwa katika operesheni zake hizo, vikosi vya ulinzi vya Yemen vimeshambulia jumla ya vyombo 49 vya kivita zikiwemo manowari, meli za kivita za kushambulia, boti za kivita na meli za kubebea ndege za kivita.
Jeshi la Yemen ambalo limekuwa bega kwa bega na Wapalestina wa
Ghaza tangu ulipoanza uvamizi na mauaji ya kimbari yanayofanywa na jeshi
katili la Kizayuni dhidi ya Wapalestina hao; na likiwa hadi sasa
limetiwa hasara kubwa kutokana na mashambulizi ya ndege za kivita za
Marekani na Uingereza, limetangaza kuwa, operesheni za vikosi vya ulinzi
vya nchi hiyo dhidi ya meli za Israel au zinazoelekea bandari za
utawala huo katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu zitasitishwa pale tu
uvamizi na mzingiro waliowekewa watu wa Palestina katika Ukanda wa Ghaza
vitakapokomeshwa.
Wizara ya Afya ya Palestina imetoa ripoti mpya ya idadi ya
Wapalestina waliouliwa shahidi na kujeruhiwa kutokana na jinai za
utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza na kueleza kuwa tangu
yalipoanza mashambulizi ya jeshi la utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda
wa Ghaza, hadi sasa watu elfu 39,677 wameuawa shahidi na wengine 91,645
wamejeruhiwa.../
Comments
Post a Comment