COP29: Nchi za visiwa vidogo zashutumu 'dharau' kwa rasimu ya makubaliano
COP29: Nchi za visiwa vidogo zashutumu 'dharau' kwa rasimu ya makubaliano
Muungano wa nchi za visiwa vidogo (Aosis) umeshutumu siku ya Ijumaa Novemba 22 "dharau" kwa "watu walio katika mazingira magumu", baada ya kuchapishwa kwa rasimu ya makubaliano katika mkutano wa 29 wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi (COP29) inayotoa dola bilioni 250 kila mwaka katika ufadhili wa hali ya hewa kutoka nchi tajiri.
Imechapishwa:
“Tunasihi dhamiri ya kiadili ya wale wanaodai kuwa washirika wetu ili wawe upande wetu, wanyooshe mkono wao kwetu na wasituache,” lashutumu kundi hili la visiwa katika Pasifiki, Karibea au kutoka Afrika.
Katika COP29, toleo la makubaliano ya mwisho halikumridhisha yeyote... na hasa nchi za Kusini. Hawawezi “kubaki mateka wa biashara [hizi] za kisiasa,” amesema waziri wa Colombia.
Nchi tajiri hatimaye zimeweka kadi zao katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa hali ya hewa mjini Baku kwa kupendekeza dola bilioni 250 kwa mwaka kwa ajili ya hatua za hali ya hewa. Pendekezo "halikubaliki kabisa", rais wa kundi la Afrika amejibu siku ya Ijumaa katika mkutano wa 29 wa Umoja wa Mataifa kuhusu tabianchi (COP29) huko Baku.
Comments
Post a Comment