DRC: Vita vyasababisha kuongezeka kwa bei ya vyakula katika masoko ya Goma
DRC: Vita vyasababisha kuongezeka kwa bei ya vyakula katika masoko ya Goma
Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kufuatia mashambulizi ya waasi wa M23, bei ya chakula imepanda katika mji wa Goma, mji mkuu wa mkoa wa Kivu Kaskazini, ambao una zaidi ya wakazi milioni moja. Vyakula vinavyotumiwa zaidi, kama vile viazi na maharagwe, vimeshuhudia bei yake ikiongezeka maradufu katika masoko ya Birere na Kituku, ambayo wakazi wa Goma wanategemea.
Imechapishwa:
Kutoka kwa mwanahabari wetu huko Goma, Héritier Baraka
Katika soko la bidhaa za chakula la Birere, wafanyabiashara wanalalamikia ukosefu wa wateja. Lakini pia kodi zinazotozwa na makundi yenye silaha, ambayo yameongeza bei nchini DRC. “Ubora huu wa maharage ya rangi mbalimbali huuzwa kwa dola 65 kwa kila gunia, maharagwe mekundu kwa dola 70, mfuko wa viazi unauzwa dola 95! », anasema mmoja wao, Bahufite Ntihemuka.
Kutokana na kushuka kwa uzalishaji katika maeeo ya Masisi, Rutshuru na kufungwa kwa barabara, bidhaa za chakula zinazidi kuwa adimu huko Goma. Mfanyabiashara wa jumla wa viazi katika soko hili la Birere, Neema Ngarukiye ana shida ya kuuza bidhaa zake, ambazo ni ghali sana, na pia ana shida kuzipata: “Kabla ya vita, nilipakua lori kumi kwa siku. Leo, siwezi hata kuuza lori moja. "
Kupanda maradufu kwa bei kwenye soko
Maharage, mboga mboga, viazi, vyakula vinavyotumiwa zaidi mjini Goma vimeshuhudia bei yake ikiongezeka maradufu. Mfumuko huu wa bei unadhuru uwezo wa kununua wa familia. Akiwa ameketi juu ya jiwe la volkeno mbele ya biashara yake ndogo ya nguo za wanawake katika eneo la Ndosho, magharibi mwa Goma, Céline Mbuhu anasema kwamba leo hii, anapata shida kulisha watoto wake:
“Tunaishi kwa shida kwa sababu ya vita vya M23. Hapo awali, hata nikiwa na watoto wangu saba, ningeweza kununua chakula cha jioni kwa urahisi kwa faranga 5,000 za Kongo [$1.7]. Leo, haiwezekani. "
Ndizi na makaa ya mawe huvuka Ziwa Kivu
Tangu kusonga mbele kwa waasi wa M23 ambao walizunguka mji wa Goma, usambazaji wa chakula umekuwa mgumu. Kutoka kilomita zaidi ya kumi , katika mwambao wa Ziwa Kivu, soko la Kituku limekuwa tumaini pekee la kuendelea kuishi kwa wakaazi wa Goma. Bidhaa za chakula hutokea katika eneo la Masisi, Minova na Buzi-Bulenga, katika mkoa wa Kivu Kusini, na zinafika kwa wingi kila Jumatatu na Alhamisi, siku za soko. Zawadi Emilliane ni mfanyabiashara anayevuka Ziwa Kivu kuuza ndizi zake:
"Ninaleta angalau mikungu kumi ya ndizi na ninapata pesa nyingi, ninapata faranga 10,000 za CFA," anasema kwa furaha. Hata makaa ya mawe yaliyokuwa yanatoka Masisi na Rutshuru sasa yanatoka Kalehe. "Kuna shughuli nyingi katika soko la Kituku," anaona msimamizi wa soko hilo Chance Kanane. Uuzaji wa mkaa unaweza kuzidi magunia 5,000 siku za Jumatatu na Alhamisi, siku za soko. "
Wakati wa kusubiri mwisho wa vita na kufunguliwa tena kwa barabara ya Goma-Sake-Minova, njia ya baharini kwenye Ziwa Kivu imekuwa muhimu kwa ajili ya kusambaza chakula kwa wakazi wa Goma, wanaokabiliwa na wingi wa idadi ya na watu waliohama makazi yao kutoka maeneo jirani.
Comments
Post a Comment