EU yamrejesha nyumbani balozi wake Niger

 

EU yamrejesha nyumbani balozi wake Niger

Saleh Mwanamilongo
Dakika 29 zilizopita

Idara ya kidiplomasia ya EU imesema kulikuwa na "tofauti kubwa" juu ya shutuma zilizotolewa na viongozi wa kijeshi wa Niger.

https://p.dw.com/p/4nNHk
Nakili kiunganishi
EU yamrejesha nyumbani balozi wake Niger kufuatia mzozo kuhusu msaada wa kiutu
EU yamrejesha nyumbani balozi wake Niger kufuatia mzozo kuhusu msaada wa kiutuPicha: Denis Doyle/Getty Images

Ijumaa, wizara ya Mambo ya Nje ya Niger iliushutumu Umoja wa Ulaya kwa kutenga dola milioni 1.3 katika misaada ya kibinadamu kwa mashirika kama vile Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu na Baraza la Wakimbizi la Danmark bila kushauriana na mamlaka. Viongozi wa Niger walisema hatua hiyo haikuzingatia kanuni za uwazi na ushirikano mzuri baina ya pande mbili.

Kwa upande wake EU iliwashutumu viongozi wa Niger kutumia misaada ya kibinadamu kwa malengo ya kisiasa. Fedha hizo ni msaada uliotakiwa kuelekezwa kwa waathirika wa mafuriko makubwa yaliyoikumba nchi hiyo ya Sahel.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan