Haiti yamwitisha balozi wa Ufaransa baada ya matamshi 'yasiyokubalika' ya Emmanuel Macron
Haiti yamwitisha balozi wa Ufaransa baada ya matamshi 'yasiyokubalika' ya Emmanuel Macron
Wizara ya Mambo ya Nje ya Haiti imetangaza hivi punde siku ya Alhamisi, Novemba 21, kuwa imemwitsha balozi wa Ufaransa na kupinga matamshi yaliyochukuliwa kuwa yasiyokubalika ya Rais Emmanuel Macron, akiwashutumu maafisa wa Haiti kuwa "wajinga kabisa."
Imechapishwa:
Mkuu wa diplomasia ya Haiti Jean-Victor Harvel Jean-Baptiste alielezea siku ya Alhamisi mchana kwa mwanadiplomasia wa Ufaransa Antoine Michon "ghadhabu ya Nguvu ya Mpito mbele ya kile anachokiona kuwa ishara isiyo ya kirafiki na isiyofaa ambayo inastahili "kurekebishwa", kulingana na taarifa ya wizara kwa vyombo vya habari ambayo ilibainisha kuwa balozi wa Ufaransa "alitambua kwamba haya yalikuwa maoni ya bahati mbaya" yaliyotolewa kando ya mkutano wa kilele wa G20 huko Rio.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliwashutumu maafisa wa Haiti kwa kuwa "wajinga kabisa" ambao walimtimua malakani Garry Conille, aliyeteuliwa Waziri Mkuu miezi mitano iliyopita kujaribu kuleta utulivu nchini mwake, kulingana na video iliyopigwa Jumatano huko Rio ambayo inasambazwa kwenye mitandao ya kijamii. Katika video hii iliyorekodiwa pembezoni mwa mkutano wa G20 kabla ya kuondoka kwake kuelekea Chile, nje ya uwepo wa waandishi wa habari, rais wa Ufaransa anajibu, kulingana na wasaidizi wake, raia wa Haiti ambaye alimhoji "mara kwa mara" akimshtumu yeye na Ufaransa " kuwajibika kwa hali ya Haiti”.
"Kuna ukweli, ni Wahaiti walioua Haiti, kwa kutia mbele biashara ya madawa ya kulevya," Emmanuel Macron alijibu.
“Na huko walichokifanya, Waziri Mkuu alikuwa mtu wa maana, nilimtetea, wakamtimua! », aliongeza kwa kurejelea kutimuliwa kwa Garry Conille na baraza la mpito la rais wa Haiti.
Comments
Post a Comment