Iran kufanya mazungumzo ya Nyuklia na mataifa ya Ulaya

 

ran kufanya mazungumzo ya Nyuklia na mataifa ya Ulaya

Saleh Mwanamilongo
Dakika 20 zilizopita

Iran imetangaza kuwa itafanya mazungumzo ya nyuklia na nchi tatu za Ulaya — Ufaransa, Ujerumani, na Uingereza — wiki ijayo mjini Geneva.

https://p.dw.com/p/4nNHl
Nakili kiunganishi
Serikali ya Iran kufanya mazungumzo ya Nyuklia na mataifa matatu ya Ulaya mjini Geneva
Serikali ya Iran kufanya mazungumzo ya Nyuklia na mataifa matatu ya Ulaya mjini GenevaPicha: Lisi Niesner/REUTERS

Iran imetangaza kuwa itafanya mazungumzo ya nyuklia na nchi tatu za Ulaya — Ufaransa, Ujerumani, na Uingereza — wiki ijayo mjini Geneva.

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kufanyika Novemba 29 na yatahusu mzozo wa mpango wa nyuklia wa Iran, kufuatia azimio lililopitishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la udhibiti wa nyuklia dhidi ya Iran. Iran ilijibu azimio hilo kwa hatua kama vile kuwasha vinu vipya na vya kisasa vya urutubishaji wa urani.

Serikali ya Rais Masoud Pezeshkian inatafuta suluhu ya mkwamo wa nyuklia kabla ya kuapishwa kwa Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump, Januari.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan