Kiongozi wa upinzani Msumbiji aweka masharti ya mazungumzo

 

Kiongozi wa upinzani Msumbiji aweka masharti ya mazungumzo

Saa 3 zilizopita

Kiongozi wa upinzani Msumbiji amesema atakubali mwito wa rais wa mazungumzo baada ya ghasia kali za baada ya uchaguzi kwa masharti ikiwemo yafanyike kwa njia ya mtandao na mchakato wa kisheria dhidi yake usitishwe.

https://p.dw.com/p/4nLK9
Nakili kiunganishi
Mgombea wa upinzani Msumbiji Venâncio Mondlane
Mondlane, mgombea wa kujitegemea, anayesema uchaguzi ulichakachuliwa ili kukipa ushindi chama cha Nyusi cha FrelimoPicha: Alfredo Zuniga/AFP

Rais Filipe Nyusi amemualika Venancio Mondlane ofisini kwake mjini Maputo Novemba 26 baada ya vifo vya watu kadhaa katika ukandamizaji wa polisi dhidi ya maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 9.

Soma pia:Upinzani nchini Msumbiji kuomboleza vifo vya watu 50 kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi

Mondlane, mgombea wa kujitegemea, anayesema uchaguzi ulichakachuliwa ili kukipa ushindi chama cha Nyusi cha Frelimo, inaaminika aliondoka nchini kwa hofu ya kukamatwa au kushambuliwa, lakini haijulikani aliko.

Amesema katika hotuba aliyoitoa kwenye ukurasa wa facebook, kuwa wako tayari kwa mazungumzo ya kweli na yasiyokuwa na mitego. Maafisa wamemfungulia mashitaka ya jinai na kiraia dhidi yake, ikiwemo uharibifu uliosababishwa wakati wa maandamano ya wafuasi wake, ambayo yamepelekea akaunti zake za benki kufungiwa.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan