Maporomoko ya ardhi yawaua watu tisa Kivu ya Kusini

 

Maporomoko ya ardhi yawaua watu tisa Kivu ya Kusini

Saleh Mwanamilongo
Saa 4 zilizopita

Watu tisa wamekufa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia maporomoko ya ardhi huko Nyabibwe katika jimbo la Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://p.dw.com/p/4nMrP
Nakili kiunganishi
Maporomoko ya ardhi yawaua watu tisa Kivu ya Kusini, Mashariki mwa Kongo
Maporomoko ya ardhi yawaua watu tisa Kivu ya Kusini, Mashariki mwa KongoPicha: GLODY MURHABAZI/AFP

Watu tisa wamekufa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia maporomoko ya ardhi huko Nyabibwe katika jimbo la Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Thomas Bakenga, mkuu wa mtaa wa Kalehe amesema nyumba kadhaa zilisombwa na mafuriko ya mvua na matope katika mji wa wakulima wa Nkubi na kuharibu mashamba kadhaa.

Waliofariki ni pamoja na Mama na watoto wake saba ambao nyumba yao ilifukiwa na tope. Na msichana mwengine alifariki katika kambi ya wakimbizi ya eneo hilo.

Kwa upande wake, Delphin Birimbi, mkuu wa asasi za kiraia katika mtaa wa Kalehe, amesema mvua hiyo ilisababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu.

Mvua zinazoendelea kunyesha mara kwa mara husababisha mafuriko na vifo vya watu katika baadhi ya maeneo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan