Marekani yazuia ndege za kiraia kwenda nchini Haiti

 

Marekani yazuia ndege za kiraia kwenda nchini Haiti

Saa 2 zilizopita

Marekani imezuia ndege zote za kiraia kwenda nchini Haiti kwa mwezi mmoja, siku moja baada ya ndege moja ya Marekani kushambuliwa.

https://p.dw.com/p/4mwiL
Nakili kiunganishi
Haiti | Uwanja wa ndege wa Port-au-Prince
Uwanja wa kimataifa wa ndege katika mji wa Port-au-Prince ukiwa katika hali ya utulivu katikati ya mapigano ya magenge ya wahalifu nchini HaitiPicha: Odelyn Joseph/AP Photo/picture alliance

Ndege moja ya Marekani ilishambuliwa ilipokuwa ikikaribia kwenye mji mkuu wa Haiti, muda mfupi baada ya Waziri Mkuu mpya kuapishwa.

Hatua hiyo ya Mamlaka ya Anga ya Marekani imefikiwa baada ya ndege ya shirika la Spirit iliyokuwa ikiwasili Port-Au-Prince ikitokea Florida kushambuliwa kwa risasi na kulazimika kubadilisha njia na kwenda Jamhuri ya Dominica.

Hadi jana Jumanne, Haiti ilisalia kama taifa lililotengwa na ulimwengu, wakati uwanja wake mkuu wa ndege ukiwa umefungwa na milio ya risasi ikiendelea kusikika maeneo mbalimbali.

Waziri Mkuu mpya Alix Didier Fils-Aimealiapishwa siku ya Jumatatu akichukua nafasi ya Garry Conille aliyeteuliwa mwezi Mei.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan