Mwendesha mashtaka wa ICC achunguzwa kwa unyanyasaji kingono

 

Mwendesha mashtaka wa ICC achunguzwa kwa unyanyasaji kingono

Saa 7 zilizopita

Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Uhalifu, ICC ya mjini The Hague, Päivi Kaukoranta amesema wameanzisha uchunguzi dhidi ya Mwendesha mashtaka mkuu Karim Khan anayetuhumiwa kwa unyanyasaji wa kingono.

https://p.dw.com/p/4mtny
Nakili kiunganishi
 Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC, Karim Khan
Mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya uhalifu ya mjini The Hague, Karim Khan kuchunguzwa kwa madai ya unyanyasaji wa kingonoPicha: Peter Dejong/REUTERS

Kaukoranta amesema jana Jumatatu kwamba chombo huru kitachunguza madai hayo ili kuhakikisha mchakato huo unakuwa huru, usioegamia upande wowote na wa haki.

Madai hayo yaliibuliwa mwezi Oktoba, lakini muhanga, ambaye ni mtumishi kwenye ofisi ya Khan aliripotiwa kuupinga uchunguzi na hakutaka kuyazungumzia madai hayo, hivyo kufanya uchunguzi huo kusitishwa.

Khan mwenyewe ameyapuuza madai hayo akisema hayana msingi na kuzihakikishia mamlaka kwamba yuko tayari kushirikiana na wachunguzi.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan