Niger yalifutia leseni shirika la NGO la Ufaransa la Acted

 

Niger yalifutia leseni shirika la NGO la Ufaransa la Acted

Saa 2 zilizopita

Utawala wa kijeshi nchini Niger jana Jumanne umefuta leseni ya shirika lisilo la kiserikali la Acted la Ufaransa kufanya kazi nchini humo, katikati ya mvutano na mtawala wake huyo wa kikoloni.

https://p.dw.com/p/4mwie
Nakili kiunganishi
Niger | Jenerali Abdourahamane Tchiani | Kiongozi wa serikali ya kijeshi
Utawala wa Niger umekuwa ukichukua hatua kadha wa kadha ikilenga kuondoa uhusiano na mataifa hasa ya magharibi tangu serikali ya kijeshi ilipoingia madarakaniPicha: ORTN/Télé Sahel/AFP/Getty Images

Acted imekuwa ikifanya kazi nchini Niger tangu 2009, ikijishughulisha zaidi na watu waliokimbia makazi yao katika taifa hilo lililokumbwa na ghasia za waasi.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Niger ilitoa taarifa hiyo, bila ya kueleza sababu za kufuta leseni hiyo. Shirika jingine la APBE pia lilikumbwa na kadhia kama hiyo ya kufutiwa leseni.

Tangu utawala wa kijeshi ulipoingia madarakani Julai 2023, ulianza kuipa kisogo Ufaransa, na kuanzisha uhusiano na wanaharakati wenzao Burkina Faso na Mali, pamoja na Urusi.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan