Pakistan yasitisha huduma za simu na intaneti

 

Pakistan yasitisha huduma za simu na intaneti

Saleh Mwanamilongo
Dakika 3 zilizopita

Hatua hiyo imechukuliwa wakati wafuasi wa Waziri Mkuu wa zamani Imran Khan aliyefungwa jela wakijiandaa kwa maandamano katika mji mkuu.

https://p.dw.com/p/4nNHn
Nakili kiunganishi
Pakistan yasitisha kwa kiasi huduma za simu na intaneti kabla ya maandamano ya upinzani
Pakistan yasitisha kwa kiasi huduma za simu na intaneti kabla ya maandamano ya upinzaniPicha: Faridullah Khan/DW

Serikali na Wizara ya Mambo ya Ndani zilitoa tangazo kwamba huduma za mtandao na simu zitaendelea kwenye maeneo mengine ya nchi, bila kutaja maeneo husika na muda itakaodumu hatua hiyo.

Wafuasi wa Imran Khan wanataka kiongozi wao aachiwe huru. Khan amekuwa gerezani kwa zaidi ya mwaka mmoja na ana zaidi ya kesi za jinai 150 dhidi yake.

Hata hivyo bado Lakini anabaki kuwa maarufu na chama chake cha kisiasa cha Pakistan Tehreek-e-Insaf au PTI, kinasema kesi hizo zinachochewa kisiasa.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan