Serikali ya Mali yafunga kituo cha televisheni cha kibinafsi
Serikali ya Mali yafunga kituo cha televisheni cha kibinafsi
Sudi Mnette
Saa 14 zilizopitaSaa 14 zilizopita
Mamlaka ya Kijeshi ya Mali imekifunga kituo cha utangazaji cha kibinafsi baada ya mshirika wake mwenza ambayo pia inaendeshwa kijeshi Burkina Faso kulalamikia utangazaji wake.
https://p.dw.com/p/4nLjS
Nakili kiunganishi
Russland Mali Militärjunta untersagt politische Aktivitäten | Assimi Goita
Rais wa Mali Assimi Goita akihudhuria mkutano wa kilele wa Urusi na Afrika huko Saint Petersburg, Urusi, Julai 29, 2023.
Picha: Alexander Ryumin/TASS Host Photo Agency via REUTERS
Matangazo
Afisa mmoja wa kituo hicho aliyezungumza kwa msaharti ya kutotajwa jina lake aliliambia shrika la habari la AFP kwamba mamlaka ya mawasiliano ya Mali ilizuia leseni ya Joliba TV News kuanzia tarehe 26 Novemba. Hatua hiyo inafuatia malalamiko yaliyowasilishwa dhidi ya kituo hicho Novemba 12 na mamlaka ya mawasiliano ya Burkina Faso kuhusu maoni yaliyotolewa na mwanasiasa wa Mali Issa Kaou N'Djim kuhusu serikali ya Burkina Faso yenyewe. Anatarajiwa kushtakiwa kwa kumkashifu hadharani mkuu wa nchi ya kigeni Desemba 23. Mataifa hayo mawili ya Afrika Magharibi yanatawaliwa na tawala za kijeshi tangu mapinduzi ya mwaka 2020 na 2022, yakiungana na Niger inayoongozwa pia kijeshi ambayo yameunda shirikisho la Muungano wa Nchi za Sahel (AES).
Comments
Post a Comment