Steinmeier aahirisha safari kushughulikia mzozo wa nyumbani

 

Steinmeier aahirisha safari kushughulikia mzozo wa nyumbani

Saa 7 zilizopita

Rais wa Shirikisho la Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ameahirisha safari yake ya Saudi Arabia wiki ijayo ili kufanya mazungumzo na viongozi wa kisiasa nchini humo, kutokana na mzozo ulioikumba serikali mjini Berlin.

https://p.dw.com/p/4mtl3
Nakili kiunganishi
Rais wa Shirikisho, Steinmeier
Rais wa Shirikisho la Ujerumani Frank-Walter-Steinmeier ameahisirisha ziara yake ya Saudi Arania ili kushiriki mazungumzo ya mzozo wa kisiasaPicha: Sebastian Gollnow/dpa/picture alliance

Mazungumzo hayo yamepangwa kufanyika baada wiki hii na kundi la awali la viongozi wa chama cha Kansela Olaf Scholz cha Social Democrats, SPD na chama cha kihafidhina cha Christian Social Union, CSU.

Mapema jana Jumatatu, Waziri wa Mambo ya Nje Annalena Baerbock alielezea umuhimu wa kuwepo kwa utaratibu mzuri wa mabadilishano nchini Ujerumani na hasa kwa kuzingatia ushindi wa Donald Trump.

Kansela Scholz alitangaza kuitisha kura ya imani ya bunge mwezi Januari baada ya serikali yake ya muungano kuvunjia wiki iliyopita, suala ambalo hata hivyo hatarajiwi kuliwasilisha hapo kesho atakapolihutubia bunge.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan