Sudan: Baraza la usalama la UN kuchukua hatua dhidi ya pande hasimu

 

Sudan: Baraza la usalama la UN kuchukua hatua dhidi ya pande hasimu

Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanathathmini azimio lililoandaliwa na Uingereza, kutaka jeshi na wanamgambo wa RSF nchini Sudan, kusitisha mapigano na kuruhusu misaada ya kibindamu kuwafikia mamilioni ya watu walioathiriwa na mzozo huo.

Urusi  na China. Uingereza inataka azimio hilo kupigiwa kura haraka iwezekanvyo.
Urusi  na China. Uingereza inataka azimio hilo kupigiwa kura haraka iwezekanvyo. REUTERS - David Dee Delgado
Matangazo ya kibiashara

Azimio hilo linahitaji kuungwa mkono kwa kura tisa bila ya kuwepo kwa kura ya turufu kutoka wajumbe wakudumu ambao ni kutoka Marekani, Ufaransa, Uingereza, Urusi  na ChinaUingereza inataka azimio hilo kupigiwa kura haraka iwezekanvyo.

Itakumbukwa kuwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha maazimio mawili ya awali kuhusu Sudan mwezi Machi na kutoa wito wa kusitishwa mara moja kwa uhasama wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Maelfu ya raia wa Sudan wamepoteza makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya jeshi na wapiganaji wa RSF.
Maelfu ya raia wa Sudan wamepoteza makazi yao kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya jeshi na wapiganaji wa RSF. © AP

Haya yanajiri wakati huu, ikiwa ni mara ya kwanza kwa wataalam wa Umoja wa Mataifa kuzuru mji wa Port Sudan, kwa siku tatu, kujionea hali ilivyo hasa kwenye jimbo la Darfur.

Umoja wa Mataifa umesema karibu watu milioni 25, nusu ya wakazi wa Sudan wanahitaji msaada huku njaa ikishuhudiwa katika kambi za wakimbizi na watu milioni 11 wamekimbia makazi yao. Karibu milioni 3 ya watu hao wamekwenda nchi zingine kuwa wakimbizi.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan