Trump kumteua Huckabee kuwa balozi wa nchini Israel

 

Trump kumteua Huckabee kuwa balozi wa nchini Israel

Saa 2 zilizopita

Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametangaza kumteua Mike Huckabee kuwa balozi wa taifa hilo nchini Israel.

https://p.dw.com/p/4mwiJ
Nakili kiunganishi
Mrepublican, Mike Huckabee
Mike Huckabee, kiongozi wa kiimani aleyegeukia siasa, katika picha iliyopigwa mwaka 2016 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habariPicha: APImages

Trump amemtaja Huckabee kama mtumishi makini wa umma, gavana na kiongozi wa kiimani kwa miaka mingi akisema anaipenda Israel na waru wa Israel pia wanampenda.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Saar alipongeza uteuzi huo wa Huckabee ambaye aliwahi kusema hakuna kitu kama uvamizi, linapokuja suala la maeneo ya Kipalestina.

Huckabee mwenye miaka 69, aliwahi kuwania nafasi ya kugombea urais mara mbili katika chama chake cha Republican na amekuwa na misimamo mikali dhidi ya haki za wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan