Ukraine na Urusi zazima mashambulizi kadhaa ya droni

 

Ukraine na Urusi zazima mashambulizi kadhaa ya droni

Saleh Mwanamilongo
Saa 4 zilizopita

Jeshi la anga la Ukraine limesema limedungua zaidi ya droni 10 za Urusi zilizorushwa kuelekea mji wa Kyiv usiku wa kuamkia Jumapili.

https://p.dw.com/p/4nMrO
Nakili kiunganishi
Ukraine na Urusi zazima mashambulizi kadhaa ya ndege zisizo na rubani
Ukraine na Urusi zazima mashambulizi kadhaa ya ndege zisizo na rubaniPicha: U.S. Army/ABACA/picture alliance

Kwa upande wake, Wizara ya Ulinzi ya Urusi iliripoti kuwa zaidi ya droni 30 za Ukraine zilidunguliwa katika ardhi yake usiku wa kuamkia Jumapili.

Mkuu wa mkoa wa Kursk magharibi mwa Urusi amesema droni ishirini na saba na makombora mawili vilirushwa kwenye anga ya mkoa huo na wanajeshi wa Ukraine.

Wakati huohuo, Kampuni ya gesi ya Urusi Gazprom imesema itasafirisha leo Jumapili mita za ujazo milioni 42 za gesi kwenda Ulaya kupitia Ukraine.

Comments

Popular posts from this blog

Mali: Wanachama wa Azimio la Machi 31 watoa wito wa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa

Raia wa Somaliland, eneo lililojitenga na Somalia wanashiriki uchaguzi mkuu

Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan