Urusi: Vita vya Ukraine vinachukua 'mkondo wa kidunia', anasema Vladimir Putin
Urusi: Vita vya Ukraine vinachukua 'mkondo wa kidunia', anasema Vladimir Putin
Vladimir Putin amezungumza katika hotuba ya televisheni mnamo Novemba 21, 2024, ambapo amethibitisha utumiaji wa kombora la masafa ya kati lisilo na kichwa cha nyuklia, lililotumiwa kushambulia jiji la Dnipro, nchini Ukraine. Hafichi nia yake ya kufanya shambulio katikanchi ambazo silaha zake zinatumiwa na Ukraine nchini Urusi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Rais wa Urusi Vladimir Putin ametangaza Alhamisi, Novemba 21, kwamba vikosi vyake viliishambulia Ukraine kwa kombora jipya la masafa ya kati, baada ya kushambulia mji wa Dnipro ambapo kombora hilo halikuwa na kichwa cha nyuklia. "Wahandisi wetu wameliita Oreshnik," Vladimir Putin amesema katika hotuba kwa taifa. Kulingana na rais wa Urusi, shambulio hili ulimelenga "eneo la kiwanda cha jeshi la Ukraine".
Katika hotuba yake iliyochukua chini ya dakika 10, rais wa Urusi ameshutumu mashambulio mawili ya hivi majuzi yaliyofanywa na Ukraine katika ardhi ya Urusi kwa kutumia makombora ya Marekani ya ATACMS na ya Uingereza ya Storm Shadow na kuzingatia kwamba mzozo wa Ukraine umechukua "tabia ya kimataifa", kwa kuwajibisha Watu wa Magharibi ambao waliidhinisha matumizi ya makombora ya Marekani na Ulaya kwenye ardhi ya Urusi.
"Tangu [makombora haya yaliporushwa nchini Urusi], na kama tulivyosisitiza mara kwa mara (hapo awali), mzozo uliochochewa na nchi za Magharibi nchini Ukraine ulichukua sura ya [mgogoro] wa asili ya ulimwengu," rais wa Urusi amesema. , akibainisha hata hivyo kwamba mashambulio ya makombora ya Magharibi yaliyorushwa na Ukraine kuelekea ardhi ya Urusi yameshindwa.
"Katika tukio la kuongezeka kwa vitendo vya fujo, tutajibu kwa nguvu sawa"
Rais wa Urusi Vladimir Putin amehakikisha kuwa nchi yake iko "tayari kwa matukio yote" katika mzozo kati ya Ukraine na washirika wake wa Magharibi.
"Siku zote tumekuwa tayari, na bado tuko tayari, kutatua shida zote kwa njia za amani, lakini pia tuko tayari kushughulikia maendeleo yoyote," amesema katika hotuba hii iliyotangazwa kwenye runinga ya Urusi. "Ikiwa kuna mtu bado ana shaka, haina maana. Daima kutakuwa na jibu,” ameonya, bila kuficha nia yake ya kupiga nchi ambazo silaha zao zinatumiwa na Ukraine nchini Urusi.
"Tunajiona kuwa ndani ya haki zetu za kutumia silaha zetu dhidi ya mitambo ya kijeshi ya nchi ambazo zinaidhinisha matumizi ya silaha zao dhidi ya mitambo yetu. Na katika tukio la kuongezeka kwa vitendo vya uchokozi, tutajibu vivyo hivyo,” amesema katika hotuba iliyowashangaza wengi.
Kulingana na Vladimir Putin, kombora hili la hypersonic haliwezi kushindwa.
"Hakuna njia leo ya kukabiliana na silaha kama hizo. Makombora hayo yanalenga kwa kasi ya Mach 10, au kilomita 2.5 hadi 3 kwa sekunde. Mifumo ya ulinzi wa anga inayopatikana sasa ulimwenguni na mifumo ya ulinzi wa makombora iliyoundwa na Marekani huko Ulaya haizuii makombora haya. Hili limetengwa,” amebainisha.
"Maendeleo yanatia wasiwasi", yasema Umoja wa Mataifa
Utumiaji wa Moscow wa kombora jipya la masafa ya kati kushambulia Ukraine ni "maendeleo mapya yanayotia wasiwasi", msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema Alhamisi.
"Haya ni maendeleo mapya yanayotia hofu na yanayotia wasiwasi, yote yanakwenda katika mwelekeo mbaya," Stéphane Dujarric amewaambia waandishi wa habari. Ametoa wito kwa pande zote kuchukua "hatua za haraka za kupunguza mzozo ili kuhakikisha ulinzi wa raia na miundombinu muhimu ya kiraia," akirejelea wito wa Katibu Mkuu Antonio Guterres wa kukomesha vita hivi kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
Comments
Post a Comment