Kikao cha OIC cha mjini Jeddah na majukumu ya nchi za Kiislamu
Kikao cha OIC cha mjini Jeddah na majukumu ya nchi za Kiislamu Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC imeamua kuitisha kikao dha dharura mjini Jeddah, Saudi Arabia wakati huu ambapo Iran na kambi ya muqawama inajiandaa kutoa majibu makali kwa Israel kutokana na vitendo vya kigaidi vya utawala wa Kizayuni. Ali Bagheri, Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, jana Jumatano asubuhi aliondoka mjini Tehran kuelekea Jeddah, akiongoza ujumbe wa Iran kwa ajili ya kushiriki katika kikao hicho cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa OIC. Kikao hicho cha OIC ni cha kujadili matokeo mabaya ya jinai za Wazayuni dhidi ya wananchi wa Palestina na vilevile jinai ya utawala haramu wa Kizayuni ya kumuua shahidi Sheikh Ismail Haniyeh, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS. Jinai nyingine ya Israel ...